Mazingira Yasiyoepukika kwa Mwanamke Kutoa Maamuzi - NOA Swahili

Mobile Menu

Posts Title Display

Top Ads

Responsive Leaderboard Ad Area with adjustable height and width.

More News

logoblog

Mazingira Yasiyoepukika kwa Mwanamke Kutoa Maamuzi

Apr 28, 2019

 









                                                                        Loading...






Kuna
mambo ambayo wataalamu wengi wamekuwa wakiongelea katika maisha hasa
yanayohusiana na hisia, tunapokuja kwenye swala la kutaka kufanya
maamuzi tunashauriwa sana kuepuka kufanya maamuzi unapokuwa na hisia
fulani, hii inaweza kukuletea matokeo  chanya au hasi lakini mara nyingi
unakuwa haujategemea kupata matokeo hayo kulingana na hali uliyokuwa
nayo.

Kwa wanawake, hii huwa ngumu kwao kwa sababu kuna hali 
ambazo aidha kwa kupenda au kutokupenda anaweza kujikuta tu akifanya
maamuzi bila kujali yataleta matokeo gani baadae.





Kwa
kumsikiliza pia moja ya wataalamu wa mahusiano kutoka chuo kikuu cha
Dar Es Salam , Chris Mauki anasema kuwa kuna hali ambazo mwanamke hata
ufanye nini inakuwa ngumu kwake kuacha kufanya maamuzi pengine apate mtu
wa karibu sana kuweza kuzipinga hatua zake.

Baadhi ya hali hizo zinazoweza kumfanya ashindwe kuacha kufanya maamuzi ni pamoja na :-


  • Akiwa
    mpweke – akiwa na kiu ya kuliwazwa kwenye upweke wake haangalii huyu ni
    mume wa mtu, mchumba wa mtu, mzazi wa mtu. Yeye anachotaka upweke wake
    uishe

  •  Akiwa desparate (mwenye kiu ya kuolewa) – mwanamke akiwa
    kwenye hali hii, basi mwanaume yoyote kwake ni potential husband, awe
    mume wa mtu au la, akifikia hapa hajali mambo ya kupima afya, mambo ya
    dini au imani, vigezo na masharti vyote vinafukiwa ardhini.

  •  Akiwa
    na kiu ya mtoto – Hapa hajaliwi mtu inajaliwa mbegu tu. Kila akiona
    mwanaume anamwona kama baba mtoto wake, hapa haliangaliwi penzi tena
    bali mbegu za mtoto. Hapa hata kama ana imani ya kuhamisha milima
    atakuwa tayari kwenda kwa mganga pale anapoona maombi hayafanyi kazi.
    Mtoto atatafutwa come what may, come sun come rain


Hali yako
na mapito yako yasikufanye ushushe standards zako. Ndio maana taji hata
siku moja haitolewi mwanzoni bali mwishoni. Yeye avumiliaye atavikwa
taji –


No comments:

Post a Comment